Katika dunia inayobadilika kila siku, kuna jambo moja halibadiliki ;uaminifu wa Mungu. Tunapohisi tumepotea, tumeachwa, au tumekata tamaa, tunaweza kushikilia ahadi hii kuu: “Maana Bwana ni mwema; fadhili zake ni za milele, na uaminifu wake hudumu vizazi na vizazi.” (Zaburi 100:5)
Mungu si mwanadamu ambaye anaweza kusema na kutosheleza nusu. Kila neno lake ni la kweli. Alikuwa mwaminifu kwa Ibrahimu, Musa, Ruthu, na hata kwa wana wa Israeli waliokosa mara nyingi. Huyo huyo yuko nawe leo, na hata milele.
Uaminifu wa Mungu hutupa amani, hutujaza matumaini, na kutuhakikishia kuwa hatuko peke yetu katika mapambano ya maisha.
Andiko la Kimaandiko:
“Maana Bwana hutelekeza watu wake, wala hawaachi urithi wake.” — Zaburi 94:14
Nukuu ya Roho ya Unabii:
“Mungu hana kosa kamwe. Yeye ni mwaminifu. Ahadi zote zilizo katika Neno Lake ni za hakika.” — Prophets and Kings, uk. 164
Tafakari uaminifu wa Mungu katika maisha yako yale aliyokupitisha jana na yuko pamoja nawe leo. Mwaminifu Yeye aliyeahidi; atatimiza.